Hii si haki, utetezi wa wanyonge uko wapi, miaka 50 ya uhuru, na bado porojo nyingi tuu
Kauli hiyo ilitolewa jijini Dar
es Salaam jana, na Kamishina wa Tume hiyo, Bernadeta Gambishi, wakati
alipokuwa akizindua mradi vitabu (Vitini),vya maboresho ya sheria.
Alisema kwa kuzingatia hayo
kunaweza kuharakisha upatikanaji wa haki katika makundi yote ya kijamii
nchini, kusimamia maadili na uweled wa maofisa wa sheria, pia ukuzaji
wa uhuru wa mahakama.
Gambishi alisema kimsingi mradi huo una malengo makuu sita ambayo yatatekelezwa kwa kupitia mkakati wa Kati.
Akiyataja baadhi maeneo hayo,
kuwa ni pamoja na Mfumo bora wa sheria kitaifa: lengo hilo linasimamiwa
na Tume ya kurekebisha sheria nchini kwa kushirikiana na taasisi
nyingine washirika.
Haki za Binadamu na usimamizi
wa haki hili linasimamiwa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora na
upatikanaji wa haki kwa walio na uwezo mdogohilo linasimamiwa na
Taasisi zisizo za Kiserikali (NGO’S), mfano mmoja ni Chama cha Wana
Sheria Nchini (TLS).
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Sheria,
Reginald Makoko, alisema bado Watanzania wengi wanakabiliwa na uwelewa
mdogo wa sheria hali inayowafanya baadhi yao kupoteza haki zao.
Hata hivyo, tatizo hilo kwa sasa
limepungua kutokana kuwepo kwa vyama vyama vya kisheria ambavyo vinatoa
msada wa kisheria bure , malalamiko mengi kuwasilishwa huko.
No comments:
Post a Comment