Monday, January 14, 2013

Mikopo ya chuo kikuu -Mitaa Yetu |









Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma - UDOM wamegoma kuingia madarasani wakipinga kile walichodai kuwa ni hatua ya bodi ya mikopo ya elimu ya juu nchini kuchelewesha mikopo wanayostahili kupata.

Polisi mkoani Dodoma wamelazimika kutumia nguvu za ziada kuwatawanya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma,UDOM waliokuwa wanaandamana kwenda ofisi ya Waziri Mkuu mjini Dodoma kuwasilisha madai yao.

Dokta Nsekela amewataka wanafunzi hao kuwasilisha hati za madai yao katika ofisi yake na kuahidi kulitatua tatizo hilo ndani ya muda wa siku saba.

lakini baada ya siku saba, tatizo halikututuliwa, na baadaye wanafuzi 900 walifukuzwa na wengine kushatikwa -

No comments:

Post a Comment