John Mnyika blogspot- Uzinduzi wa hopitals Sinza- Mitaa Yetu
11 Desemba
2012 Nimeshiriki uzinduzi makabidhiano ya jengo la huduma za mama na mtoto katika
hospitali ya Sinza (ipo Sinza-Palestina) kwa msaada wa Korea ikiwa ni sehemu ya kuboresha huduma za
afya.
Ipo haja ya kuongeza watumishi wa afya ikiwemo madaktari kwa kupanua wigo
wa elimu kwa ujenzi wa Chuo Kikuu MUHAS, eneo la Kwembe Mloganzila.
Hata hivyo,
nilitarajia Rais Kikwete angeeleza serikali ilivyojipanga kuboresha maslahi
ya madaktari kwa kurejea taarifa ya
kamati ya huduma za jamii iliyoundwa baada ya mgomo wa madaktari ili kuepusha
kasi ya madaktari kwenda nchi za nje,
badala yake Rais ametoa kauli nyingine tata.
Aida, Rais amepotoshwa kuwa
wanasiasa wa upinzani wamepinga ujenzi wa MUHAS na kuahidi fidia ya usumbufu.
Ukweli ni kuwa aliyewaahidi wananchi fidia ya ardhi ni aliyekuwa Waziri wa
Ardhi, Bwana John Chiligati mnamo mwaka 2009 na 2010 kwa ajili ya CCM kupata
kura kwenye uchaguzi za serikali ya mitaa na Uchaguzi Mkuu. Wananchi wanachodai
ni waliyoahidiwa na serikali.
shukurani zako John Mnyika, http://mnyika.blogspot.com/
No comments:
Post a Comment