Monday, January 14, 2013

shule za sekondari tanzania- Mitaa yetu







Na Joachim Mushi
Rukwa
UJENZI wa Shule za Sekondari kwa kila Kata maarufu kama ‘sekondari za kata’ katika mikoa anuai umeongeza vituko kwenye sekta ya elimu kwa baadhi ya maeneo kwani kutokana na upungufu mkubwa wa walimu hasa wa masomo ya sayansi na lugha baadhi ya shule zimefuta masomo hayo kinyume na taratibu za mitaala.
Miongoni mwa mikoa iliyokubwa na kadhia hiyo ni Rukwa, Wilaya ya Nkansi ambako baadhi ya shule hizo zimekata tamaa baada ya kukosa walimu wa sayansi na kulazimika kufuta masomo ya sayansi na kubaki na yale ya sanaa, licha ya kwamba nayo si yote yenye walimu kwenye shule hizo.

No comments:

Post a Comment